Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Taarifa Mpya
Zanzibar Port Authority (ZPC) — 06 Mar 2026 @ Amani stadium
Lango Kuu la Uchumi Zanzibar

Karibu Shirika la Bandari Zanzibar

Tunajenga bandari za kisasa zinazounganisha Zanzibar na ulimwengu, tukichochea uchumi wa buluu na maendeleo ya kijamii.

ZPC Port

1997

Mwaka wa Kuanzishwa

Unguja & Pemba

Maeneo Tunayohudumia

100% Salama

Usimamizi wa Kimataifa

ZPC Building
29+ Mwaka
SISI NI NANI?

Shirika Linaloongoza kwa Mageuzi ya Bandari

Shirika la Bandari Zanzibar (ZPC) ni taasisi ya kiserikali iliyoanzishwa kwa Sheria ya mwaka 1997 ikiwa na mamlaka kamili ya kusimamia rasilimali zote za bandari visiwani Unguja na Pemba.

Kama sehemu ya mpango wa SMZ kurekebisha uchumi, ZPC imekuwa daraja muhimu la kibiashara, ikihakikisha huduma bora za upakiaji na utunzaji wa mizigo.

MWELEKEO WETU

Dira na Dhamira ya ZPC

Tunaongozwa na malengo thabiti ya kuifanya Zanzibar kuwa kitovu cha biashara Afrika Mashariki.

Dhamira Yetu

Kutoa huduma za bandari kwa ufanisi wa hali ya juu na kuitikia mahitaji ya wateja kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya kiuchumi.

Dira Yetu

Kuwa bandari zinazoongoza kwa utoaji wa huduma bora na za ushindani katika ukanda wa Bahari ya Hindi.